Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje

Mamlaka ya  Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje

Historia

Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uwekezaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) ni Taasisi ya Serikali inayofanya kazi zake chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. EPZA ilianzishwa kufuatia marekebisho ya sheria ya programu ya Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (Export Processing Zones – EPZ) ya mwaka 2006, ili kusimamia utekelezaji wa programu ya EPZ. Mwaka 2011 majukumu ya EPZA yaliongezwa na kufanya EPZA kusimamia Mpango ambao ni mpana wa Maeneo Maalum ya Kiuchumi (Special Economic Zones – SEZ). Hii ni kufuatia marekebisho ya sheria za EPZ na SEZ ya mwaka 2011, yaliyofanya EPZ kuwa sehemu ya programu ya SEZ.

Malengo ya EPZA ni kuhamasisha uwekezaji wa viwanda kwa uzalishaji wa bidhaa za kuuza nje ya nchi ili kuongeza pato la fedha za kigeni, kuongeza fursa za ajira, usindikaji wa maligafi za ndani na kuvutia teknolojia mpya.

Majukumu ya EPZA ni pamoja na kutwaa na kumiliki Maeneo Maalum ya Kiuchumi, kujenga miundombinu, kutoa leseni za uwekezaji za EPZ na SEZ, kuhudumia wawekezaji kabla na baada ya kupata leseni na kutangaza fursa za uwekezaji ndani ya Maeneo Maalumu ya Kiuchumu.

Programu ya Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZ) ilianzishwa kufuatia kutungwa kwa sheria ya Maeneo ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZ) ya mwaka 2002. Programu hii inahamasisha uwekezaji wa viwanda vinavyouza nje ya nchi vilivyopo katika maeneo maalum yaliyotengwa kwa lengo la kukuza ushindani wa kimataifa na hatimaye kukuza uchumi wa nchi.

Programu ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi (Special Economic Zones - SEZ) ilianzishwa kufuatia kutungwa kwa sheria ya Maeneo Maalum ya Kiuchumi ya mwaka 2006. Programu hii inahamasisha uwekezaji kwenye sekta mbalimbali kwa ajili ya mauzo ya ndani na nje ya nchi, ambapo programu ya EPZ ni sehemu ya programu ya SEZ. Utekelezaji wa programu ya SEZ ulianza rasmi mwaka 2011 baada ya sheria za EPZ na SEZ kufanyiwa marekebisho na kanuni za SEZ kutungwa.


BODI YA WAKURUGENZI EPZA

  • Waziri anayehusika na Viwanda ambaye ni Mwenyekiti;
  • Mwanasheria Mkuu;
  • Katibu Mkuu wa Wizara inayohusika na Fedha;
  • Katibu Mkuu wa Wizara inayohusika na Nishati;
  • Katibu Mkuu wa Wizara inayohusika na Maji;
  • Katibu Mkuu wa Wizara inayohusika na Mamlaka za Mitaa;
  • Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango;
  • Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Mapato Tanzania;
  • Kamishna wa Ardhi;
  • Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Tanzania; na
  • Rais wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda, na Kilimo Tanzania.
  • Mkurugenzi Mkuu wa EPZA ni Katibu wa Bodi ya EPZA.